BAADHI YA MAMBO YANAYO SAIDIA KATIKA TOBA


1.) Kuwa na ikhlasi kwa ajili ya Allah Azza Wa jallah. na kuelekea kwake.
Ikhlasi kwa ajili ya Allah ni dawa yenye manufaa zaidi. Pindi mja akiwa na ikhlasi kwa ajili ya Mola wake, na akawa ni mkweli katika kutafuta toba, basi Allah atamsaidia juu ya jambo hilo, atakuwa nae na atamuondoshea vizuizi na vipingamizi katika njia ya toba.


2.) Kutokuwa na matumaini makubwa juu ya dunia na kukumbuka Akhera. 
  • Mja pindi atakapo tambua ufupi wa maisha ya duniani,na uharaka wa kuondoka kwake. 
  • Na akatambua ya kwamba dunia ni shamba kwa ajili ya akhera, 
  • Na akatambua ya kwamba dunia ni fursa ya kuchuma thawabu kwa ajili ya akhera,
  • Na akakumbuka neema za milele zilizopo akhera,
  • Na akakumbuka yale yaliyo motoni miongoni mwa  adhabu ziumizazo.
Wakati huo atapunguza kujiachia katika matamanio ya nafsi,na atajirejea kwa kufanya matendo mema dhidi ya uovu alio utanguliza.

3.) Kujishughulisha na mambo yenye manufaa na kujiepusha na upweke na kukaa bure pasina ya shughuli. Kwani kukaa bure pasina ya shughuli kunapelekea kupata/kuambatana na marafiki waovu, hali itakayo sababisha kuporomoka kitabia na kukosa maadili, kutokana na kuambatana na marafiki waovu.

Na pindi mja atakapo jishughulisha na mambo yenye manufaa Duniani na Akhera, basi itapungua hali yake ya kukaa pasina ya shughuli,na hatopata nafasi ya kufanya maovu na uharibifu.

4.) Kujiepusha na vishawishi vya maasi na kila kile chenye kukumbusha maasi. Kama vile:
  • Kutizama filamu chafu,
  • kusikiliza miziki,
  • kusoma magazeti ya udaku pamoja na majarida ya riwaya zenye kuchochea maasi.
Kama inavyo takiwa kujiepusha na kila sababu zinazo weza kumkumbusha maasi kama vile marafiki vijiwe na makempu.

5.) Kusuhubiana {kuambatana} na watu wema na kujiepusha na waovu. Kwani kusuhubiana na wema huuisha moyo na hupelekea kuwaiga watu wema. Na kusuhubiana na waovu kunapelekea kuyaona maovu kuwa ni mema na mema kuyaona kuwa ni maovu. Kwani rafiki humvuta rafiki yake katika kila jambo.

6.) Daima kukumbuka madhara ya madhambi na maasi.
Kwani miongoni mwa madhara yake ni kunyimwa elimu, kupunguziwa riziki na kukosa utulivu wa moyo. Pamoja na kufanyiwa uzito katika mambo yako, kuhisi kiza katika moyo, udhaifu wa mwili na kuharamishiwa matendo mema.
           
Maasi hupanda katika moyo mbegu za maasi mengine, na husababisha kuichukia toba kidogo kidogo,mpaka inafutika katika moyo wa mja fikra ya toba.Mwenyezi Mungu Mtukufu
atulinde na hayo.

7.) Kushikamana na dua: Kama vile kumuomba Allah akuepushe na maasi,akukinge na maasi au akutoe katika maasi. Kwani dua ni katika sababu kubwa za kujiepusha na maasi na ni dawa yenye kufaa zaidi.

Nayo{Dua} ni adui wa mabalaa huyazuia na huyaponya na huyapunguza na kuyaondoa.

KIMBUNGA CHA SANDY NA MTAZAMO WA KIISLAMU

Kimbunga cha Sandy kinatarajiwa kutua katika Ardhi ya Mashariki ya Marekani likiwemo jiji la New York wakati wowote kuanzia hivi sasa, kimbunga hicho kinawafanya watu karibu milioni 50 waishi katika hali ya wasi wasi mno, kwetu sisi Waislamu matukio kama haya yana ibra, hutukumbusha kawmu kama vile za ‘Aad na Thamud, hutukumbusha watu mbali mbali ambao baada ya kufuru na uovu, Allaah aliwapelekea adhabu, inatukumbusha As-hab ul Ayka, As-habu al Hijri, Kawmu Tubba, Fir’awn na watu wa Misri, Kawmu Lut na watu waliomkanusha Nabii Nuuh (‘alahyi salam) Kwa hakika Kimbunga  cha Sandy kina mafunzo makubwa kwetu. 

Habib al Mustafa (صلي الله عليه وسلم) siku moja aliona wingu likitanda Madina, wingu katika jangwa si hali ya kawaida kwa vile ni sehemu yenye uchache wa mvua kwa kiasi kikubwa. Hivyo Mtume (صلي الله عليه وسلم) uso ulimbadlika kiasi kwamba 'Aisha (رضي الله عنه) aliona wazi wazi jinsi uso wa Mtume (صلي الله عليه وسلم) ulivyojawa na khofu, 'Aisha (رضي الله عنه) akamuuliza Mtume juu ya jambo gani lililomtia khofu. Mtume akamjibu kuwa watu waliotangulia kabla yake waliona wingu baada ya ukame wa muda mrefu, wakalifurahia wakidhani ni dalili ya mvua, kumbe wingu lile lilikuwa na adhabu ya Allaah (عز وجل), Miongoni mwa watu hao ni As-hab al Ayka. 

Utangulizi wa Tafsiri ya Qur'ani


BISMILLAAHI RAHMAANI RAHIIM
Elimu ya tafsir ya Qur’ani ni katika elimu muhimu sana. Kwani elimu hii hupelekea kufahamu maneno, matamshi na ibara za Qur ani tukufu, kujifunza hukumu mbali mbali za kisheria na kufikia malengo yaliyo kusudiwa na  na Qur ani.

Maana ya tafsiri kilugha: Tafsir kama neon la kiarabu lina maana ya ubainifu na  uwazi.
Na maana ya tafsiri kiistwilaah: Ni elimu ambayo makusudio yake ni kupelekea kufahamu kitabu cha Mwenyezi Mungu Mtukufu kilicho shushwa kwa Mtume wake Muhammad (rehema na amani ziwe juu yake) na kubainisha maana yake na kutoa hukumu zake na hekima zake. Au kwa kifupi ni Kubainisha maana za Qur’ani tukufu.

MAANA YA TWAHARA NA UMUHIMU WAKE KATIKA SALA


Twahara katika lugha maana yake ni kujisafisha/usafi. Tunapozungumza twahara katika Uislamu ni kuondoa uchafu na vyenye kuchafua, hii ni sehemu ya usafi wa kimwili au mahala au kivazi. Lakini pia twahara ina upande wa kiimani au tuseme usafi wa ki’akida. Na Allaah anatuambia katika Qur’aan:

خُذْ مِنْ أَمْوَالِهِمْ صَدَقَةً تُطَهِّرُهُمْ وَتُزَكِّيهِم بِهَا وَصَلِّ عَلَيْهِمْ ۖ إِنَّ صَلَاتَكَ سَكَنٌ لَّهُمْ ۗ وَاللَّهُ سَمِيعٌ عَلِيمٌ 
Chukua sadaka katika mali zao, uwasafishe na uwatakase kwazo, na uwaombee rehema. Hakika maombi yako ni utulivu kwao. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia Mwenye kujua. [9:103]

Bila ya shaka yoyote twahara itakayotokana na sadaqa itakuwa sio twahara ya kimwili bali ni twahara ya kuitakasa mali kiimani.

FIQ-HI YA TWAHARA - UTANGULIZI


Shukrani zote zina mstahiki Allaah, Mola Mlezi wa viumbe wote. Rehma na amani zimshukie Mtume wa Allaah na watu wake na sahaba zake, pamoja na wote wenye kufuata mwenendo wake mpaka siku ya qiyamah.
Uislamu ni dini ya kujitoharisha; ni  dini yenye kusisitiza mno kwenye suala la usafi, usafi wa moyo na hata usafi wa nje; yaani mwili na mazingira. Dini hii imetoa ufafanuzi wa hali ya juu kuhusu mambo yote tunayoyahitaji katika suala la twahara,  Uislamu umeweka wazi juu ya kanuni zote  ambazo zinamnufaisha mwanadamu katika maisha yake, hakuna ambacho ni chenye manufaa katika maisha na Uislamu umekiacha, twahara ni moja katika ya mambo yenye manufaa makubwa kwa mwanadamu ndio maana Uislamu ukasisitiza utekelezaji wake.

MAZINGATIO KATIKA HIJRAH YA MTUME (rehma na amani juu yake)


Bila shaka wengi wetu tumesoma au kusikia kuhusiana na Hijra(kuhama) ya mtume kutoka Makka na kuelekea Madina. Hapa ndipo ilipo anza tarehe ya kiislamu. Katika safari hii ya mtume kuna mazingatio mengi sana, leo hii tutazungumzia baadhi ya haya mazingatio:

1: Mazingatio ya uhamaji:
Mwenyezi Mungu alitoa idhini kwa Mtume wake na  Waumini kuhama toka Makkah kutokana na madhara mbali mbali waliyo kuwa wakiyapata kutoka kwa makafiri wa Kiquraysh. Katika haya madhara ilikuwa ni kuwazuia waislamu kuisimamisha dini yao, wakateswa na kuadhibiwa vikali.

MWAKA MPYA WA KIISLAMU(1433)


Tarehe 26/11/11 ni siku inayoafikiana na  tarehe moja  ya mwezi Muharram, yaani mwezi wa kwanza wa kiislamu, kwa hiyo tumeingia mwaka mpya wa kiislamu.Tumetoka katika Mwaka wa 1432 na tumeingia 1433.
Idadi ya miaka hii ni tokea kuhama kwa mtume kutoka Makka na kuelekea Madina. Bila shaka kuna mazingatio makubwa sana juu ya kuhama Huku kwa mtume, mazingatio ambayo tutayazungumzia InshaaAllah.
Waislamu hatuna sherehe maalumu ndani ya siku hii inayo tambulika kisheria tokea enzi za mtume, masahaba zake na mpaka hivi sasa. Bali siku hii huadhimishwa kwa kukumbuka kipindi hiki ambayo baada yake uislamu ulipata dola ya kujitegemea na waislamu kuwa na uhuru wa kufanya watakavyo tofauti  na kipindi walichokuwa Makkah. Yaani dola ya Uislamu wa umma huu wa Mtume Muhammad ilianza tarehe 1/1/1 Hijria baada ya Waislamu kuhamia Madinah.

YAA UKHTA HAARUN!


UTANGULIZI
Shukrani zote zinamsatahiki Mwenyezi Mungu Mola mlezi wa viumbe wote, Rehma na amani zimshukie Mtume Muhammad na ali zake na Sahaba zake pamoja na wote wenye kufuata mwenendo wake mpaka siku ya mwisho.
Wenye kuipinga Qur’aan hutoa madai kuhusu aya hii kwamba: Qur'aan inamwita Maryam Ukhta Haarun (Dada yake Haarun) wakati watu wawili hawa hawakuishi wakati mmoja, yaani wamepishana miaka takriban 2000. Kwa hiyo Qur’aan imefanya kosa la Kihistoria.

Lengo la makala hii ni kuthibitisha kuwa Qur’an hapa haikufanya kosa bali wenye madai haya ama hufanya makusudi kwa lengo la kupotosha ukweli au hawakuelewa aya hii.
UFAFANUZI
Mwenyezi Mungu anatuambia katika Qur’aan tukufu aya ya 19:28 ninanukuu

يَا أُخْتَ هَارُونَ مَا كَانَ أَبُوكِ امْرَأَ سَوْءٍ وَمَا كَانَتْ أُمُّكِ بَغِيًّا 
Ewe dada yake Haarun! Baba yako hakuwa mtu muovu, wala mama yako hakuwa kahaba.

Baadhi ya Du'aa za Kumuombea aliyetangulia mbele ya haki

Du’aa katika Qur’aan na Sunnah ambazo mtoto anaweza kumuomba mzazi wake aliyetangulia mbele ya haki pamoja na kuwaombea maiti wengine waislamu:

رَبَّنَا اغْفِرْ لِي وَلِوَالِدَيَّ وَلِلْمُؤْمِنِينَ يَوْمَ يَقُومُ الْحِسَاب  

Rabbana-ghfir liy waliwaalidayya walil Mu-uminiyna yawma yaquumul hisaab.

“Mola wetu! Unighufirie mimi na wazazi wangu wote wawili, na Waumini, siku ya kusimama hisabu” (Ibraahiym: 41) 
رَّبِّ ارْحَمْهُمَا كَمَا رَبَّيَانِي صَغِيرًا
Rabbir-hamhumaa kamaa rabbayaaniy swaghiyraa.

“Mola wangu! Warehemu kama walivyonilea utotoni.  (Al-Israa: 24)

رَبَّنَا اغْفِرْ لَنَا وَلِإِخْوَانِنَا الَّذِينَ سَبَقُونَا بِالإِيمَانِ وَلاَ تَجْعَلْ فِي قُلُوبِنَا غِلًّا لِّلَّذِينَ آمَنُوا رَبَّنَا إِنَّكَ رَؤُوفٌ رَّحِيمٌ  

FUNGA ZA SUNNA


Duniani ni sehemu ya kuchuma pasipo na hesabu na kesho, siku ya mwisho ni hesabu pasipo ya kuchuma. Kwa hiyo inatakiwa muumini azitumie fursa mbali mbali ili kuhakikisha ya kwamba siku ya mwisho hesabu yake mbele ya Allah anakuwa ni nyepesi.
Sasa ni mwezi mmoja na siku chache tangu kumalizika kwa mwezi mtukufu wa Ramadhani, mwezi ambao tumeonja ladha za ibaada, ikiwemo ibaada ya funga.
Tukumbuke ya kwamba ibada yafunga si mwezi mtukufu wa Ramadhani na sitatush shawwaal tu bali kuna funga  nyingine ambayo  ni sunna kuzifunga na kuweza kujipatia malipo ya hali ya juu.
Mtume rehma na amani ziwe juu yake anatueleza katika hadithi Al Qudsy iliyo pokelewa na Abu Hurayra (Allah amridhie)
عَنْ أَبِيْ هُرَيْرَةَ رَضِيَ الْلَّهُ عَنْهُ قَالَ : قَالَ رَسُوْلُ الْلَّهِ - صَلَّىَ الْلَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ - إِنَّ الْلَّهَ قَالَ: مَنْ عَادَىْ لِيَ وَلِيا فَقَدْ آَذَنْتُهُ بِالْحَرْبِ ، وَمَا تَقَرَّبَ إِلَيَّ عَبْدِيَ بِشَيْءٍ أَحَبَّ إِلَيَّ مِمَّا افْتَرَضْتُ عَلَيْهِ ، وَمَا يَزَالُ عَبْدِيَ يَتَقَرَّبُ إِلَيَّ بِالْنَّوَافِلِ حَتَّىَ أُحِبَّهُ ، فَإِذَا أَحْبَبْتُهُ كُنْتُ سَمْعَهُ الَّذِيْ يَسْمَعُ بِهِ ، وَبَصَرَهُ الَّذِيْ يُبْصِرُ بِهِ ، وَيَدِهِ الَّتِيْ يَبْطِشُ بِهَا ، وَرِجْلَهُ الَّتِيْ يَمْشِيَ بِهَا ، وَإِنْ سَأَلَنِيْ لَأُعْطِيَنَّهُ ، وَلَئِنْ اسْتَعَاذَنِيْ لَأُعِيْذَنَّهُ (رَوَاهُ الْبُخَارِيُّ)

Namna ya Kufanya Tathmini Baada ya Ramadhani

Tunamshukuru kwa dhati kabisa Allah sub-hanahu wa ta'ala kwa kutuwezesha kufika tulipo fika katika mwezi huu wa Ramadhani, pia rehma na amani zimshukie Mtume, pamoja watu wake na sahaba zake na wale wote wenye kufuata mwenendo wake mpaka siku ya qiyama. Na tunashuhudia kwamba hapana Mola anayestahiki kuabudiwa kwa haki isipokuwa Allah na Muhammad ni mja na Mtume wake.


Mwezi mtukufu wa Ramadhani ndio umefikia ukingoni, wengi ni wenye huzuni kwani ingawa ni mwezi mmoja tu, wamejenga mazoea makubwa ya kufanya mambo mbali mbali ambayo hatuyapati katika miezi mingine, mikusanyiko ya pamoja katika milo ya iftaar, misikiti kujaa, itikafu, qiyamul layl  na du’a za kuomba maghfira kama vile
 (اللَّهُمَّ إِنَّكَ عَفُوٌّ تُحِبُّ الْعَفْوَ فَاعْفُ عَنِّيْ)
Haya ni baadhi tu ya mambo ambayo wengine yanawatoa machozi kwani hatuna uhakika wa kuwa hai mpaka mwezi wa Ramadhani mwakani.

Wakati tukiwa na majonzi kufuatia kuondokewa na mwezi huu yaliyochanganyika na furaha ya sherehe za ‘Idil Fitwr, la muhimu zaidi ni kufanya tathmini juu ya mafanikio tuliyoyapata baada ya mwezi wa Ramadhani. Ili tuweze kufanya tathmini sahihi hatuna budi kufahamu nini tunatakiwa kukifikia baada ya Ramadhani. Tunachotakiwa kukifikia kimeelezewa kwenye Qur’ani katika aya ambayo Allaah ‘azza wa jall ametufaradhishia kufunga, Allaah ta’ala anatuambia:
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا كُتِبَ عَلَيْكُمُ الصِّيَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكُمْ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ 
Enyi mlio amini! Mmeandikiwa Swawm, kama waliyo andikiwa walio kuwa kabla yenu ili mpate kuwa wenye taqwa.
Kwa hiyo lengo la kufaradhishiwa swawm au funga ni kuwa na taqwa. Suala la kujiuliza ni ‘taqwa ni nini?’

Laylatul Qadr

Laylatul Qadr kilugha, maana yake ni usiku wenye nguvu au usiku wenye kudra au usiku wa cheo kitukufu, ni usiku maalum ambao unapatikana mara moja tu katika kila mwaka ndani ya mwezi wa Ramadhani. Huu ni usiku ambao Allaah ta’ala anatuambia  katika kitabu chake kitukufu kuwa Qur’ani imeteremshwa, Allaah ta’ala  anatuarifu:-
إِنَّا أَنزَلْنَاهُ فِي لَيْلَةِ الْقَدْرِ
Hakika Sisi tumeiteremsha (Qur'ani) katika Laylatul Qadri, Usiku wa Cheo Kitukufu.

Ramadhani: Salafi Swaalih na Ukarimu na Sadaka


Sadaka ndani ya mwezi mtukufu wa Ramadhani ni bora kulikoni sadaka katika miezi ya kawaida. Na ndio maana mtume "swalla llahu alayhi wasallama" akauita mwezi huu ya kwamba ni mwezi wa kuliwazana. Kwani masikini pia katika funga zao hupatwa na njaa na kiu, na mikononi mwao hawana kile kitakacho watosheleza, basi pindi wanapo patikana watu wanao wapatia sadaka na kuwafanyia ukarimu, nao hufarijika na kuliwazika. LEngo la kuwasaidia masikini hawa ni kumtii Allah ‘azza wa jall ndani ya mwezi huu mtukufu.

قَالَ رَسُوْلُ اللهِ صَلَّي اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: مَنْ فَطَرَ فِيْهِ صَائِمَا كَانَ كَفَّارَةَ لِذُنُوْبِهِ وَعِتْقَ رَقَبَتِهِ مِنَ الْنَّارِ وَكَانَ لَهُ مِنَ الْأَجَلِ مِثْلُ أَجْرِ الْصَّائِمِ مِنْ غَيْرِ أَنْ يَنْقُصَ مِنْ أَجْرِهِ شَيئَا 
سُنَنٌ الْتِّرْمِذِي
Anasema mtume rehema na amani ziwe juu yake (Yule mwenye kumfuturisha mfungaji katika mwezi huu wa Ramadhani basi kitendo chake hicho kitakuwa ni kafara ya madhambi yake. Na ataachwa huru na moto wa jahannam. Na atakuwa na malipo mfano wa malipo ya mfungaji, pasina ya kupungua malipo ya mfungaji japo kidogo)

PONGEZI ZA MWEZI MTUKUFU WA RAMADHAN



Assalaamu alaykum warahmatullahi wabarakaatuh
Ukurasa wa MIMI NI MUISLAMU (Facebook) wakishirikiana na Blogi ya Dinullah tunakupeni pongezi kwa kujaaliwa kuufikia  mwezi mtukufu wa RAMADHANI. Mwezi wenye kheri na Baraka mbali mbali. Mwezi ambao ni jukumu la kila mmoja wetu kuufunga. Ni furaha iliyoje kuufikia mwezi huu!
Wangapi walitamani kufikishwa mwezi huu lakini hivi sasa hatupo nao tena Hatuna budi kumshukuru kwa dhati Allaah ‘azza wa jall kwa kutufikisha tena kwenye neema hii kubwa isiyo na mfano, Alhamdulillahi ewe Allah kwa kutufikisha tena katika mwezi huu mtukufu wa  Ramadhani.

Nyakati za Futari na Daku


Inshallah tunaingia katika mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani. Katika mwezi huu Waislam huwa tuna milo miwili mikubwa badala ya ile ya kawaida. futari, yaani chakula ambacho tunakila baada ya kutua kwa jua baada ya kufunga siku nzima tangu kabla ya kuchomoza kwa jua na daku, chakula tunachokila kabla ya kuingia kwa sala ya alfajiri.
Uislamu haujaacha kuhimiza na kuelekeza namna ya utekelezaji wa kila jambo ikiwemo nyakati za daku na futari. Katika suala la kufungua au kufuturu Uislam unahimiza kwamba ni muhimu kuwahi kufungua mara tu baada ya kuingia wakati, yaani mara baada ya kutua au kuzama kwa jua. Hili linathibitishwa katika hadithi iliyosahihi.