Kuihimiza Familia Kusali

Shukrani zote zinamstahiki Allah, Mola mlezi wa viumbe wote. Rehma na amani zimshukie Mtume na watu wake, na masahaba wake pamoja na wote wenye kufuata mwenendo wake mpaka siku ya qiyama. 

Kuiamrisha familia kusali ni amri ya Allaah, amri hii imewekwa wazi bilaya utata wa aina yoyote kwenye Qur’aan, Allah ta’ala anatumbia katika Surat at Ta-Ha: 
وَأْمُرْ أَهْلَكَ بِٱلصَّلَوةِ وَٱصْطَبِرْ عَلَيْهَا ۖ لَا نَسْـَٔلُكَ رِزْقًا ۖ نَّحْنُ نَرْزُقُكَ ۗ وَٱلْعَـقِبَةُ لِلتَّقْوَى ﴿٢٠:١٣٢﴾

Na waamrishe familia wako kusali, na uendelee mwenyewe kwa hayo. Sisi hatukuombi wewe riziki, bali Sisi ndio tunakuruzuku. Na mwisho mwema ni kwa mchamngu. (20:132)

Hii ina maana uikoe familia ya kutokana na adhabu ya Allah kwa kuiamrisha kusali, kuiamrisha familia kusali ndio ulikuwa mwennendo wa masahaba wengi wa Mtume (رضي الله عنهم), tuchukue mfano wa Umar ibn Al Khattab (رضي الله عنه) imesimuliwa: 

وَحَدَّثَنِي عَنْ مَالِكٍ، عَنْ زَيْدِ بْنِ أَسْلَمَ، عَنْ أَبِيهِ، أَنَّ عُمَرَ بْنَ الْخَطَّابِ، كَانَ يُصَلِّي مِنَ اللَّيْلِ مَا شَاءَ اللَّهُ حَتَّى إِذَا كَانَ مِنْ آخِرِ اللَّيْلِ أَيْقَظَ أَهْلَهُ لِلصَّلاَةِ يَقُولُ لَهُمُ الصَّلاَةَ الصَّلاَةَ ثُمَّ يَتْلُو هَذِهِ الآيَةَ {وَأْمُرْ أَهْلَكَ بِالصَّلاَةِ وَاصْطَبِرْ عَلَيْهَا لاَ نَسْأَلُكَ رِزْقًا نَحْنُ نَرْزُقُكَ وَالْعَاقِبَةُ لِلتَّقْوَى}

Amesimulia Maalik kutoka kwa Zayd ibn Aslam aliyesimulia kutoka kwa baba yake; Hakika Umar ibn Al Khattab alikuwa akisali mpaka mwisho wa usiku na aliwaamsha familia yake kusali alikuwa akiwambia “Salaah, Saalah, alwasomea aya Na waamrishe familia wako kusali, na uendelee mwenyewe kwa hayo. Sisi hatukuombi wewe riziki, bali Sisi ndio tunakuruzuku. Na mwisho mwema ni kwa mchamngu. (20:132) [Muwatta Malik, Mjeledi wa Tahajjud, mlango wa 7, Hadithi ya  259]

Aya hii ndio tunayoizungumzia hapo juu, na hivi ndivyo masahaba walivyoishi kuitekeleza Qur’aan kwa maneno na matendo. 

Faida ya kusimamisha na kuihiza familia kusimamisha salaah ni kubwa, lakini aya tunayoizungumzia imetaja faida moja., nayo ni:
لَا نَسْـَٔلُكَ رِزْقًا ۖ نَّحْنُ نَرْزُقُكَ

Sisi hatukuombi wewe riziki, bali Sisi ndio tunakuruzuku

Kuhusu sehemu hii ya aya t tutarjumu (kufasiri) maelezo ya Imam Ibn Kathir katika Tafsiri yake: “Hii ina maana ukisimamisha swali, utapata riziki kwa njia usizozitarajia” 
...وَمَن يَتَّقِ ٱللَّـهَ يَجْعَل لَّهُۥ مَخْرَجًا ﴿٢﴾ وَيَرْزُقْهُ مِنْ حَيْثُ لَا يَحْتَسِبُ ۚ وَمَن يَتَوَكَّلْ عَلَى ٱللَّـهِ فَهُوَ حَسْبُهُۥٓ ۚ إِنَّ ٱللَّـهَ بَـٰلِغُ أَمْرِهِۦ ۚ قَدْ جَعَلَ ٱللَّـهُ لِكُلِّ شَىْءٍ قَدْرًا ﴿٣﴾
...Na anaye mcha Mwenyezi Mungu humtengezea njia ya kutokea. (2) Na humruzuku kwa jiha asiyo tazamia. Na anaye mtegemea Mwenyezi Mungu Yeye humtosha. Hakika Mwenyezi Mungu anatimiza amri yake. Mwenyezi Mungu kajaalia kila kitu na kipimo chake. (65:2 -3)

Hivyo aya hii inathibitisha maelezo ya ibn Kathir kwamba pamoja na wajibu wetu wa kuitafuta riziki lakini kwa wenye taqwa na kutawakal basi Allah atawarahisishia riziki kwa njia wasizozitarajia. 

Hivyo ni muhimu kuhakikisha kwamba wanafamilia wote wanasali sala za faradhi na pia ni wajibu wako kuwahimiza kusali sala za sunnah. 

Hakika Allah ndio wakili katika kila tunalolifanya. 

Allah ndiye mjuzi zaidi